Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) imepongeza mpango wa eneo la kikanda la biashara huria FTA ulioozinduliwa mwezi Agosti 2008, kufuatia kuongezeka kwa biashara ya kikanda kutokana na utekelezaji wa mpango huo. Hata hivyo, kaimu mkurugenzi wa kamati ya maendeleo ya viwanda na biashara ya SADC Calicious Tutalife amesema, hatua pekee ya kuondoa ushuru wa forodha haitoshi katika kukuza biashara ya kikanda, na ni lazima kuondoa vizuizi dhidi ya ushindani na maendeleo anuwai ya viwanda kati ya nchi za kanda hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |