Sudan Kusini itawekeza katika nishati safi ili kuhifadhi mazingira ya nchi hiyo. Waziri wa mazingira na misitu ya nchi hiyo Josephine Napwon amesema serikali inapanga kuwekeza katika nishati safi, kufufua misitu na kilimo cha kisasa ili kuhifadhi misitu na wanyamapori kufuatia athari ya vita ya muda mrefu na mabadiliko ya hali ya hewa. Naye balozi wa China nchini Sudan Kusini Hua Ning amesema nchi hiyo inaweza kuiga uzoefu wa China katika uhifadhi wa mazingira.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |