• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Polisi wa Malawi watumia gesi ya machozi dhidi ya waandamanaji wakiwa pamoja na balozi wa Marekani

    (GMT+08:00) 2019-06-07 09:47:35

    Polisi wa Malawi wametumia gesi ya machozi kuwatawanya wafuasi wa chama cha upinzani cha MCP waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Mei 21. Msemaji wa polisi James Kadadzera amesema askari polisi walifanya hivyo bila kufahamu kuwa balozi wa Marekani nchini humo Virginia Palmer alikuwa kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho. Tarehe 27 mwezi uliopita, Tume ya uchaguzi ya Malawi ilitangaza rais Peter Mutharika ameshinda tena uchaguzi mkuu, matokeo yaliyosusiwa na wafuasi wa vyama vya upinzani, ambao wamefanya maandamano kwa njia ya amani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako