Ethiopia imesema imekamata raia wake wanne wanaoshukiwa kuwaua maofisa wa serikali za mitaa. Watu hao pia wanatuhumiwa kufanya uporoaji katika sehemu tofauti mjini Addis Ababa na maeneo ya jirani. Mwezi Disemba mwaka jana, mamlaka za Ethiopia zilikamata watu 15 waliotuhumiwa kuwaua maofisa wa serikali za mitaa katika jimbo la Oromia, na pia kuwalenga askari wa usalama na raia wa kawaida.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |