Watu zaidi 281 wamekufa katika ajali za barabarani kwenye robo ya kwanza ya mwaka huu nchini Malawi, ikiwa imeongezeka kutoka watu 234 mwaka jana wakati kama huu.
Naibu msemaji wa polisi wa Malawi Bw Thomeck Nyaude amesema katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka huu, polisi wamerekodi ajali 2,350, likiwa ni ongezeko la asilimia 143 kwa mwaka, na likiwa ni ongezeko la ajali 965 kutoka mwaka jana. Amesema kati ya ajali hizo, 215 zilikuwa mbaya, zikiwa zimeongezeka kiasi kutoka 206 kuliko mwaka jana wakati kama huo.
Bw. Nyaude amesema ajali nyingi kati ya hizo zingeeupukika kama watumiaji barabara wangekuwa makini, na kukumbusha kuwa ni wajibu wa watumiaji, kuangalia kasi, moja ya sababu zinazosababisha ajali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |