• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wasindikaji watakiwa kufuata kanuni za usafi

    (GMT+08:00) 2019-06-07 20:06:22

    Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Tanzanai imewataka wasindikaji wadogo wa chakula mkoani Mara kuzingatia taratibu na kanuni za usafi katika eneo la usindikaji, ili kuzuia vimelea vya magonjwa kuingia kwenye bidhaa wanazozalisha kwa lengo la kulinda afya ya mlaji.

    Akitoa agizo hilo mjini Musoma kwenye mafunzo ya wajasiriamali wadogo wanaosindika vyakula, Kaimu Meneja TFDA Kanda ya Ziwa Mashariki, Nuru Mwasulama, alisema ni vyema wazalishaji wa vyakula vya aina hiyo kufikisha elimu waliyopewa kwa wafanyakazi wao wanaosaidia kutengeneza vyakula hivyo.

    Alisema iwapo mfanyakazi atagundulika kuwa na maradhi yaliyotajwa hataruhusiwa kufanya kazi kiwandani mpaka atakapopona.

    Kadhalika alisema kiwanda kinatakiwa kuwa na sehemu maalumu zenye nafasi za kutosha kubadilisha nguo, maliwato na bafu ikiwamo sehemu ya kunawa mikono, na kwamba vyote vinatakiwa kukidhi mahitaji ya jinsia zote.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako