Uingereza imeanzisha kituo cha mafunzo ya kijeshi cha Baidoa, kusini magharibi mwa Somalia, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kulinda utulivu nchini humo. Ubalozi wa Uingereza huko Mogadishu umesema, kituo hicho kilichofunguliwa Jumamosi iliyopita kitatumiwa na jeshi la serikali ya Somalia SNA kutoa mafunzo kwa wanajeshi 120 kwa wakati mmoja na kulisaidia jeshi la Somalia kuboresha kiwango cha mafunzo ya kijeshi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |