Mkuu wa jeshi la Polisi mkoani Jawzjan nchini Afghanistan Bw. Abdul Wahid Wajdan amesema, vikosi vya usalama nchini humo vimewakamata wapiganaji wanane akiwemo jaji mwandamizi wa Taliban katika mkoa huo.
Wahid amesema, jaji wa Mahakama ya Taliban ya Mtaa wa Pashtun Kot wa Jimbo la Faryab Bw. Mawlawi Nasir, alikuwa akiwapeleka wapiganaji kadhaa hospitali Jumamosi wakati polisi walipomtambua na kumkamata pamoja na watu wengine saba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |