Rais John Magufuli wa Tanzania jana amewataka maofisa wapya wa ngazi ya juu wa serikali watekeleze wajibu wao katika kushughulikia matatizo ya kibiashara pamoja na mapungufu yaliyopo, na kuwaonya kuwa kama wakifanya makosa, watafukuzwa kazi.
Rais Magufuli amesema hayo baada ya kuwaapisha maofisa watatu wapya, akiwemo waziri mpya wa viwanda na biashara Bw. Innocent Bashungwa na mkuu wa Mamlaka ya Kodi Tanzania TRA Bw. Edwin Mhede.
Rais Magufuli ameeleza kusikitishwa kwake na hali ya sasa ya TRA na wizara ya viwanda na biashara, na kusema hiyo ndio sababu kubwa ya mabadiliko hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |