Rais Donald Trump wa Marekani amesema, kama bunge la Mexico halitapitisha makubaliano kuhusu uhamiaji, basi ushuru dhidi ya bidhaa zake utarejeshwa.
Ijumaa iliyopita Marekani na Mexico zilifikia makubaliano ili kuepuka kuongezwa kwa ushuru dhidi ya bidhaa zote za Mexico. Ikiwa sehemu ya makubaliano hayo, Mexico itapeleka vikosi vya ulinzi kote nchini humo ili kuzuia wahamiaji haramu, haswa mpaka wa kusini. Marekani itapanua mpango wa kuwaruhusu wanaotafuta hifadhi kubaki nchini Mexico wakati masuala yao ya kisheria yanashughulikiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |