Shirika la habari la Russia limeripoti kuwa, balozi wa Russia nchini Lebanon Alexander Zasypkin amepinga sera ya nje ya Marekani.
Bw. Zasypkin amesema Marekani inajaribu kuharibu uhalali wa kimataifa kwa kujitoa kwenye Makubaliano ya Nyuklia ya Iran, na kuongeza vikwazo vya kiuchumi, kuanzisha vita ya kibiashara, na kudhoofisha Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wapalestina, UNRWA. Amesema kuwa hatua hizo zitaleta matatizo makubwa kwa nchi mbalimbali duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |