• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • KIKAPU: Durant majanga, Raptors yaloa kwa Warriors

    (GMT+08:00) 2019-06-13 09:14:53

    Wakicheza uwanja wa nyumbani, Toronto Raptors wameshindwa kumaliza kazi waliyoianza ugenini uwanja wa Golden State Warriors wiki iliyopita waliposhinda mechi zote mbili mfululizo.

    Ushindi huo unakamilisha mechi nne za awali kwa Raptors kuongoza kwa matokeo ya 3-1 na walikuwa wanatakiwa kushinda mchezo wao mmoja uliofuata uliochezwa alfajiri ya Jumanne.

    Mchezo huo ulimalizika kwa Toronto Raptors kufungwa na Golden State Warriors kwa alama 105- 106 wakishindwa kumaliza mchezo kwa dakika moja ya mwisho na kuwaruhusu Warriors kufunga alama moja iliyoipa ushindi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako