Mashindano ya kombe la dunia kwa wanawake yanaendelea nchini Ufaransa, kwenye mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo uwanja wa Auguste-Delaune II jijini Paris, Timu ya taifa ya wanawake ya Marekani iliipiga kipigo cha mbwa koko timu ya taifa ya Thailand kwa jumla ya magoli 13-0 katika kundi F Unaweza ukasema ni kama mchezo wa netball lakini ndio soka.
Matokeo ya michezo mingine iliyopigwa jana, Sweden imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Chile, Nigeria nao wamewaonyesha soka linavyochezwa Korea Kusini kwa kuwabandika goli 2-0, huku wenyeji Ufaransa ikiibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Norway, na Ujerumani ikiipiga Uhispania goli 1-0. Leo Australia itavaana na Brazil.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |