• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Fainali za kombe la dunia kwa wanawake- Marekani yatoa kipigo cha mbwa koko, yaitandika Thailand 13-0

    (GMT+08:00) 2019-06-13 09:15:10

    Mashindano ya kombe la dunia kwa wanawake yanaendelea nchini Ufaransa, kwenye mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo uwanja wa Auguste-Delaune II jijini Paris, Timu ya taifa ya wanawake ya Marekani iliipiga kipigo cha mbwa koko timu ya taifa ya Thailand kwa jumla ya magoli 13-0 katika kundi F Unaweza ukasema ni kama mchezo wa netball lakini ndio soka.

    Matokeo ya michezo mingine iliyopigwa jana, Sweden imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Chile, Nigeria nao wamewaonyesha soka linavyochezwa Korea Kusini kwa kuwabandika goli 2-0, huku wenyeji Ufaransa ikiibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Norway, na Ujerumani ikiipiga Uhispania goli 1-0. Leo Australia itavaana na Brazil.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako