Kocha wa timu ya taifa ya Uganda (the Cranes) Sebastien Desabre amesema. Atatumia ujuzi wake wote alionao kuhakikisha wanamzuia nyota wa Misri anayecheza soka Uingereza Mohamed Salah.
The Cranes ipo kundi A pamoja na wenyeji Misri katika mashindano ya mataifa ya Afrika (AFCON 2019) yatakayofanyika nchini Misri kuanzia Juni 21 hadi Julai 9. Timu ya Uganda imepangwa kukutana na Misri katika mchezo utakaopigwa Juni 30.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |