Bingwa wa mbio za kilomita 42 za Singapore mwaka 2016, Felix Kirwa ni mwanariadha wa hivi karibuni kutoka Kenya, amefungiwa kwa miezi tisa kushiriki mashindano ya riadha kutokana na utumiaji wa dawa za kusisimua misuli iliyopigwa marufuku michezoni iitwayo Strychnine.
shirika la kusimamia uadilifu katika riadha (AIU) limesema kwamba kiwango cha Strychnine katika kipimo chake kilitofautiana na maelezo yake.
Kirwa anaingia katika orodha ya karibu wanariadha 60 wa Kenya waliopatikana wakitumia dawa za kusisimua misuli zilizopigwa marufuku michezoni tangu mwaka 2012.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |