• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • MIELEKA: John Cena awatangazia habari mbaya mashabiki wake "Bado nahitajika ila naona umri unaniacha"

    (GMT+08:00) 2019-06-14 09:10:57

    Mwanamieleka maarufu nchini Marekani, John Cena amesema kuwa kwa sasa anafikiria kustaafu kucheza mchezo huo kwa kile alichodai kuwa umri unamtupa mkono.

    Cena mwenye miaka 42, akiongea na mtandao wa TMZ, amesema, amefikiria hivyo baada ya kutazama mchezo kati ya The Undertaker na Bill Goldberg mchezo uliopigwa wikiendi iliyopita nchini Saudi Arabia.

    Mchezo huo kati ya Taker na Goldberg uliwaboa mashabiki wengi wa mieleka baada ya mahasimu hao kuonekana wote wawili kuchoka mwanzoni mwa pambano hilo.

    John Cena amesema ameshangazwa na wanamieleka hao kucheza chini ya kiwango na anajiona na yeye anaelekea huko, hivyo haoni sababu ya kuendelea kucheza mchezo huo siku za usoni.

    Hata hivyo, John Cena hajataja rasmi ni lini atatangaza kustaafu, lakini kutokana na majeraha yanayomuandama mara kwa mara huenda siku sio nyingi akatangaza adhma hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako