Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda ameipatia klabu ya Yanga eneo la kujenga uwanja wa mpira wilayani Kigamboni. Ahadi hiyo ameitoa katika hafla ya kuichangia Yanga iliyofanyika Juni 15, 2019 Jijini Dar Es Salaam. Na sasa tupate kionjo kidogo mambo tyalivyokuwa kwenye hafla hiyo na ahadi aliyoitoa Makonda. Makonda amesema anaelewa umuhimu wa timu kubwa kama hizi zinapofanya michezo katika Mkoa wao wa Dar hivyo ametafakari kama serikali na kuamua kuwapa Yanga uwanja huo. Wengine waliochangia kwenye hafla hiyo ni Bilionea Rostam Aziz, ambaye ametoa milioni 200 na Boss wa Kampuni ya GSM ametoa Milioni 300.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |