Sudan Kusini imeahidi kudumisha amani na utulivu ili kumaliza mateso ya mamilioni ya watoto kutokana na mapambano ya miaka mitano.
Waziri wa vijana, utamaduni na michezo Bibi Nadia Arop Dudi amesema, matatizo ya kiuchumi yaliyosababishwa na mapambano yameathiri vibaya maisha ya watoto hasa wa kike ambao wanaacha shule kutokana na ndoa za utotoni.
Bibi Arop pia amesema, ingawa Sudan Kusini ina sheria za kimataifa na za kikanda zinazolinda haki za watoto, lakini sheria hizo hazitekelezwi inavyopaswa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |