Uwanja huo utapanuliwa kutoka kilomita mbili zinazotumika sasa hadi kufikia kilomita 3.3, hatua itakayofanikisha ndege kubwa kutua katika uwanja huo.
Aliyasema hayo jijini Mbeya wakati wa kongamano la kuhamasisha uwekezaji katika kilimo cha mboga na matunda lililoandaliwa na Kituo cha Uwekezaji (TIC), Taasisi ya Kuendeleza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (Sagcot) na Shirikisho la Wakulima wa Mboga na Matunda (Taha).
Alisema lengo la serikali ni kuwezesha ndege za mizigo kutua na kupaa kwa urahisi na kuwarahisishia wananchi kusafirisha bidhaa zao kwenda kwenye masoko yakiwamo ya matunda na mboga.
Aidha, serikali inakusudia kuukarabati uwanja huo kwa kuweka taa ili kuwezesha ndege kutua na kupaa kwa wakati wote
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |