Prof. Mkenda aliyasema hayo alipotembelea makumbusho hayo na kujionea urithi na hazina ya taifa ambao ni pamoja na mafuvu na masalia ya binadamu wa kale au zamadamu.
Masalia hayo ni pamoja na Australopithecus, Afarensis, Zinjanthropus (paranthropus) boisei, Homo habilis, Homo erectus na Homo sapiens, yenye umri wa tangu miaka milioni 3.6 hadi miaka 200,000 iliyopita.
Alisema matangazo kwenye runinga, redio na magazeti kuhusu vitu vinavyotunzwa Makumbusho ya Taifa, yatajenga uelewa kwa wananchi kuhusu umuhimu wa makumbusho na hivyo, kufanya watu wengi kuyatembelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |