• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakulima waomba serikali iongeza bei

    (GMT+08:00) 2019-06-21 17:20:45

    Wanachama wa vyama vya ushiriki vya wakulima wanaozalisha kahawa wa Uru mkoani Kilimanjaro nchini Tanzania wameiomba serikali kusaidia kuongeza bei ya kahawa ili ifikie angalau Sh. 5,000 kwa kilo.

    Wazalishaji hao walisema bei ya sasa ni Sh. 3,000 ambayo ni ndogo ikilinganishwa na thamani ya kahawa duniani, na kwamba ongezeko la bei litawawezesha wakulima wa kahawa kuzalisha kwa wingi, kuzingatia ubora na kukuza pato lao na la taifa.

    Aidha, wameomba kurudishiwa mfumo wa kuwakopesha pembejeo za kilimo ili waweze kuzalisha kahawa nyingi zaidi na yenye tija sokoni.

    Mwenyekiti wa Muungano wa Vyama vya Ushirika Uru Njari, Felix Masao , alitoa ombi hilo alipokuwa akizungumzia hali ya uzalishaji kahawa.

    Alisema ikiwa wakuliwa watatazamwa kwa jicho la pekee wataleta mabadiliko ikiwa ni pamoja na kuondoa umaskini kwa jamii.

    Masao alisema licha ya kahawa kwa sasa kushuka bei, mwamko wa wakulima ni mkubwa ukilinganisha na kipindi cha nyuma.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako