Walisema shughuli hiyo haifai kuharakishwa kwani huenda ikaleta madhara kwa wafanyakazi husika na hatimaye kuathiri uchumi wa nchi.
Viongozi hao wamesema tangazo hilo linatolewa kabla ya serikali kuhakikisha kuwa mpango huo unahimiliwa kwenye sheria.
Kamati hiyo pia ilionya Tume ya Utumishi wa Umma (PSC) dhidi ya kutumia mpango huo kama hatua ya kuwaadhibu au kuwanyanyasa wafanyakazi wa umma.
PSC ilisema kuwa kuanzia Julai mosi mwaka huu, watumishi wa umma watakuwa wakiajiriwa kwa kandarasi ya miaka mitatu. Pia kandarasi hizo zinaweza tu kuongewa kwa miaka mingine mitatu ikiwa wafanyakazi husika watatimiza malengo ya utendakazi waliyowekewa.
Muungano wa Vyama vya Wafanyakazi (COTU) pamoja na vyama vingine vimepinga mpango huo vikidai haufai.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |