Shirika la kundeleza kilimo cha Chai nchini Kenya (KTDA) limeongeza malipo kwa wakulima kwenye maeneo ambako uchuuzi wa bidhaa hiyo unaendelea kwa wingi.
Mwenyekiti wa kitaifa wa KTDA Peter Kanyago amesema shirika hilo limeamua kuwalipa wakulima kati ya shilinhgi 17 na 18 kwa kilo moja ya chai kuanzia mwezi Juali.
Amesema hatua hiyo inafuatia mkutano na maafisa wa wizara ya kilimo.
Wakulima katika maeneo ya Murang'a, Nyamira, Kisii, Nandi, Transzoia, Vihiga na Kakamega watalipwa shilingi 17 huku wale wa Bomet na Kericho wakilipwa shilingi 18.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |