Bingwa wa zamani wa uzito wa juu Wladimir Klitschko ameokolewa na walinzi wa pwani wa Hispania baada ya boti ya kifahari aliyokuwemo kuungua moto. Bondia huyo mwenye miaka 43, ambaye amestaafu ngumi August 2017, alikuwa kwenye mapumziko katika ufukwe wa Mallorca.Tangu pambano lake la mwisho la knockout ambalo alishindwa na Muingereza Anthony Joshua Aprili 2017 Klitschko amekuwa mhadhiri wa kozi ya usimamizi kwenye chuo kikuu cha Switzerland na ameandika kitabu cha ushauri wa biashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |