Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo amefanya ziara ya ghafla mjini Kabul, Afghanistan na kujadiliana na viongozi wa nchi hiyo kuhusu mazungumzo ya amani ya Afghanistan. Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na televisheni ya Afghanitan, Pompeo alikutana na rais Ashraf Ghani na ofisa mkuu mtendaji wa serikali Abdullah Abdullah, na wamekubaliana kuwa amani ni kipaumbele cha kwanza kwa sasa, na Afghanistan haipaswi kuwa kituo cha kulea ugaidi wa kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |