Mustakabali wa uchumi wa China, sera mpya za China kwa makampuni ya kigeni, mabadiliko ya mtindo wa mitaji ya China zimeendelea kuwa mada kuu zilizojadiliwa kwenye mkutano huo. Ishara za kuzidi kufungua mlango na kushikilia mageuzi zinazotolewa na China zimepongezwa na pande mbalimbali, wageni wengi wanaoshiriki kwenye mkutano huo wana imani na matarajio kuhusu nguvu ya China na mipango ya China katika kuhimiza maendeleo ya uchumi wa dunia.
Siku hiyo waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang pia amefanya mazungumzo na wajumbe 200 wa sekta za viwanda na biashara, fedha, jumuiya ya washauri mabingwa, na vyombo vya habari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |