Mchezo wa nusu fainali ya pili ya michuano ya kombe la dunia kwa wanawake umechezwa jana jijini Paris Ufaransa inakoendelea michuano hiyo kwa Uholanzi kupata goli 1-0 dhidi ya Uswidi.
Mchezo wa fainali utazikutanisha Marekani ambayo iliifunga Uingereza 2-0 jana, na Uholanzi, mechi inayotabiriwa kuwa ya vuta nikuvute kwakuwa kila timu inataka kudhihirisha ubora wake na kunyakuwa ubingwa wa dunia wa soka la wanawake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |