Bei ya pakiti ya maziwa ya nusu lita sasa itakuwa Sh50 kutoka Sh55.
Mkurugenzi Mkuu wa New KCC Nixon Sigey anasema kampuni hiyo imeshusha bei kutokana na kuongezeka kwa usambazaji wa maziwa,hivyo basi wanasambaza manufaa hayo kwa wanunuzi ambao wamekuwa wakinunua bidhaa hiyo kwa bei za juu katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.
Alisema bei hizo mpya zilianzishwa tarehe 2 Julai na zinafaa kutekelezwa na wauzaji wa reja reja.
Sigey alisema ijapokuwa kampuni ya New KCC haijafika katika viwango ilivyokuwa miezi miwili iliyopita,viwango vya maziwa viliyopo vinatosha kubadilisha bei ya bidhaa hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |