Waasi wa Houthi wa Yemen wametangaza kuhusika na mashambulizi kadhaa dhidi ya maeneo ya kijeshi katika mkoa wa Marib unaodhibitiwa na serikali uliopo kaskazini mashariki mwa Yemen kwa kutumia ndege zisizo na rubani na makombora. Ndege hizo zililenga mfumo wa kujilinda na makombora uliomilikiwa na muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia unaounga mkono vikosi vya serikali ya Yemen dhidi ya waasi wa Houthi, huku makombora yakilenga mkusanyiko wa askari katika eneo la katikati ya Marib na kuwaua watu kadhaa wakiwemo viongozi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |