Waziri wa mambo ya nje wa Cuba Bruno Rodriguez amekosoa vikwazo vya Marekani dhidi ya kampuni ya serikali inayofanya biashara na Venezuela. Amesema Marekani haina haki ya kuchukua hatua ya upande mmoja dhidi ya mashirika yoyote ya Cuba na ya nchi nyingine yanayofanya biashara na Venezuela. Ameongeza kuwa kitendo hicho kinakiuka Sheria ya Kimataifa, kanuni zinazosimamia biashara na mashambulizi dhidi ya mahusiano na nchi zenye mamlaka huru.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |