Mchezo mwingine utakuwa baina ya Morocco na Benin, huku kesho zitapigwa mechi kati ya wenyeji Misri na Afrika Kusini nao mchezo unatolewa macho je Afrika Kusini watafanikiwa kuwaangusha Mafarao wa Misri mjini Cairo? Nigeria wao watavaana na Cameroon mjini Alexandria. Julai 7, Madagascar wataumana na DR Congo mjini Alexandria huku Algeria wao watamenyana na Guinea mjini Cairo. Julai 8 zitapigwa mechi mbili kati ya Mali na Ivory Coast mjini Suez na Ghana watakutana na Tunisia mjini Ismailia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |