Polisi wa Afghanistan wamesema soko na makazi ya raia yaliyoko mkoani Faryab, kaskazini mwa nchi hiyo yameshambuliwa kwa mizinga leo asubuhi, na kusababisha vifo vya raia wanne na wengine 36 kujeruhiwa.
Msemaji wa kituo cha polisi cha mkoa wa Faryab Bw. Abdul Karim Yurish amesema wapiganaji wa Kundi la Taliban walirusha makombora mengi. Kabla ya tukio hilo kutokea, vikosi vya usalama vilipambana kwa risasi na wapiganaji wa Kundi la Taliban. Mapambano hayo bado yanaendelea, vikosi vya usalama vinajaribu kuwafukuza waasi hao, ili kuhakikisha amani na utulivu wa eneo hilo. Kundi la Taliban bado halijasema lolote kuhusu tukio hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |