Imesema hali hiyo inayotokana na wenye nyumba wengi kutofuata sheria za ujenzi pamoja na viwango vya ubora.
Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Dk. Ludigija Bulamile, alisema watu wanaouza ramani hawaangalii wala kupima viwango vya ujenzi unaotakiwa mahali husika.
Alisema kuna maeneo hayaruhusiwi kujenga nyumba za ghorofa au nyumba kubwa kutokana na ardhi iliyopo, na wakati mwingine ardhi inakuwa na maji, hivyo kuhitaji msingi mkubwa na mchanganyiko wa zege imara. Lakini watu wananunua na kujenga kwenye maeneo hayo bila kuzingatia athari zinazoweza kutokea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |