Washindani karibu 1,400 wameingia katika nusu fainali ya shindano la ala za kichina lililoandaliwa na Shirika Kuu la Utangazaji la China CGM, ambayo itafanyika kuanzia tarehe 9 hadi 18 mwezi huu.
Washindani karibu elfu 6 kutoka miji na mikoa 20 ya China, Hong Kong, Macao, Taiwan na nchi za nje kama Mongolia, Malaysia, Japan, Singapore na Marekani wameshiriki kwenye mashindano hayo. Lengo la mashindano hayo ni kutangaza utamaduni na kusambaza elimu kuhusu muziki wa kichina.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |