Taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Marekani imesema, rais Donald Trump wa nchi hiyo amezungumza kwa njia ya simu na mwenzake wa Ufaransa Bw. Emmanuel Macron kuhusu suala la Iran.
Marais hao wawili wamejadili kuhusu jitihada zinazoendelea katika kuhakikisha kuwa Iran haitakuwa na silaha ya nyuklia, na vitendo vya Iran vya kuhujumu utulivu katika Mashariki ya Kati.
Hii ni mara ya pili kwa viongozi hao wawili kufanya mazungumzo kwa njia ya simu kuhusu suala la Iran katika wiki iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |