• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda yahitaji bilioni 100 pesa za Rwanda kusaidia nguvukazi ya kitaifa.

    (GMT+08:00) 2019-07-09 18:23:10
    Kwa zaidi ya mika mitano ijayo, kati ya mwaka wa 2019 na 2024, serikali ya Rwanda inahitaji bilioni 100, pesa za Rwanda ili kulainisha vyuo vya kiufundi na vile vya kitaalam yaani (TVET). Hii itasaidia kukuza wataalam na wafanyikazi wengine waliohitimu kutumikia taifa, huku wengine wakitumwa kufanya kazi katika mataifa ya nje. Vile vile, lengo lingine ni kuwawezesha Warwanda kujisimamia na kujiajiri.

    Kulingana na takwimu zilizopo, waajiri nchini Rwanda wamefurahishwa na nguvukazi ya warwanda kwa asilimia 78, na endapo serikali itatimiza lengo la kutoa mafunzo zaidi, asilimia hii inatarajiwa kufika 85 mwaka wa 2024.

    Baadhi ya mikakati iliyowekwa ni kuanzishwa kwa mtaala wenye ushindani mkubwa na kutoa masomo ya kiufundi kwa vijana. Serikali ya Rwanda inapania kutengeneza nafasi za ajira takriban milioni 1.5, kazi ambazo si za shambani ifikapo mwaka wa 2024. Hii ina maana kwamba kila mwaka serikali ya Rwanda itatengeneza nafasi za ajira ambazo ni zaidi ya laki mbili.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako