Shirika la habari la Syria SANA limeripoti kuwa, waziri wa mambo ya nje wa Syria Bw. Walid al-Moallem amejadiliana na mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Syria Bw. Geir Pedersen kuhusu uundaji wa kamati ya katiba.
Pande hizo mbili zimesisitiza uratibu wa mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika kuhimiza mazungumzo ya Syria ili kusaidia kurejesha utulivu na usalama nchini humo na kulinda ukamilifu wake wa ardhi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |