• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: AFDB Kuipandisha Tz daraja

    (GMT+08:00) 2019-07-11 18:44:06
    Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB), inatarajia kuipandisha daraja Tanzania kutoka katika hadhi ya kunufaika na Mfuko wa Maendeleo wa Benki (ADF) hadi kuwa na hadhi itakayoiwezesha Tanzania kupata rasilimali fedha zaidi kupitia dirisha la benki. Endapo Tz itafanikiwa kupandishwa hadhi, basi ina maana kwamba taifa hilo litanufaika na ongezeko la fedha kutoka AfDB kutoka Dola za Marekani milioni 350 kwa mwaka hadi Dola za Marekani milioni 812 kwa mwaka.

    Haya ni kwa mujibu wa mwakilishi Mkazi wa Benki hiyo Dkt Alex Mubiru. Alisema kwamba kupandishwa hadhi au daraja kunatokana na uchumi wan chi kufanya vizuri, hususani katika maeneo ya kasi ya ukuaji wa uchumi na kuwa na deni himilivu. Aidha Benki hiyo inajivunia kufanya kazi wka ukaribu na taifa la Tz, ambalo ni miongoni mwa mataifa waasisi wa Benki hiyo. Naye Waziri wa Fedha na Mipango wa Tz Dk. Philip Mango amesema kwamba Benki hiyo ina mtazamo chanya katika maendeleo ya watu na kuwa dira katika mipango ya maendeleo na kuahidi kushirikiana nao vyema katika kukuza uchumi wa Tanzania.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako