Umoja wa Ulaya umefungua makao makuu ya ujumbe wake nchini Kuwait. Katika sherehe ya uzinduzi wake, naibu waziri mkuu na waziri wa mambo ya nje wa Kuwait Sheikh Sabah Khaled Al-Hamad Al-Sabah amesema, ujumbe wa Umoja wa Ulaya nchini humo umeonyesha kuwa ushirikiano kati ya pande hizo mbili umepata mafanikio ya kihistoria. Amesema Umoja wa Ulaya ni mwenzi muhimu wa Kuwait katika biashara, uwekezaji, nishati, elimu, afya na sekta nyingine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |