Chama cha Fatah kinachoongozwa na rais Mahmoud Abbas wa Palestina kimetoa wito kwa Umoja wa Mataifa kutoa fedha zote zinazohitajika katika kazi za Shirika la Msaada na Kazi la Umoja wa Mataifa kwa Wakimbizi wa Palestina UNRWA. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika la habari la Palestina WAFA, baraza la ushauri la chama hicho limejadili kuhusu Marekani kupunguza msaada kwa UNRWA katika mkutano wake wa kawaida. Pia limetaka kuanzishwa kwa taifa huru la Palestina lenye mji mkuu Jerusalem Mashariki, hatua ambayo itakuwa msingi wa utatuzi wa mgogoro kati ya Palestina na Israel.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |