Takriban watu elfu 72 waliathirika baada ya umeme kukatika usiku wa Jumamosi huko Manhattan, New York, Marekani. Umeme ulirudishwa kwenye maeneo yote yaliyoathiriwa muda mfupi kabla ya usiku wa manane Jumamosi. Kampuni ya huduma za umeme Con Edison imeeleza kusikitishwa na tatizo hilo na kwamba uchunguzi unafanyika kujua chanzo cha tukio hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |