Rais Edgar Lungu wa Zambia amemfukuza kazi waziri wa fedha wa nchi hiyo Bibi Margaret Mwanakatwe, na taarifa iliyotokea jana usiku inasema naibu gavana wa benki kuu ya Zambia Bw. Bwalya Ng'andu anachukua nafasi yake.
Hakuna taarifa iliyotolewa kuhusiana na kufukuzwa kazi kwake, lakini Rais Lungu amempongeza kwa kazi aliyofanya tangu alipopteuliwa mwezi Februari mwaka jana.
Hata hivyo kulikuwa na shinikizo la kumfukuza kazi waziri huyo kutoka kwa wadau mbalimbali, waliodai kuwa anashindwa kusimamia vizuri uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |