Rais Donald Trump wa Marekani ameamuru kuwa, bidhaa ambazo kwa asilimia 55 zimetengenezwa Marekani ndizo pekee zinazoweza kuchukuliwa kama "Zimetengenezwa Marekani", huku akitarajia kuongeza kiwango hicho hadi asilimia 75 katika siku zijazo.
Akizungumza katika maonyesho ya bidhaa zinazotengenezwa nchini humo yaliyofanyika ikulu hapo jana, rais Trump aliliambia kundi la wanaviwanda wa Marekani kuwa, kama ikiwezekana kujenga, kulima, ama kutengeneza Marekani, nchi hiyo iko tayari kufanya hivyo.
Hii ni mara ya tatu kwa ikulu ya Marekani kufanya maonyesho ya bidhaa zinazotengenezwa nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |