Ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa imesema idadi ya watu waishio na njaa inaongezeka na mwaka jana kufikia zaidi ya milioni 820. Kwa mujibu wa Ripoti hiyo ya "Hali ya Usalama wa Chakula na Lishe Duniani kwa Mwaka 2019", baada ya miongo ya kupungua taratibu, njaa duniani inayopimwa kwa kiwango cha utapiamlo ilianza kuongezeka mwaka 2015. Ukosefu mkubwa wa usalama wa chakula umesababisha njaa, na watu wanakosa uwezo wa kupata chakula na wamelazimishwa kula chakula kidogo na kisicho na ubora.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |