Bunge la Msumbiji limepitisha sheria ya kuzuia ndoa za utotoni. Mkuu ya Tume ya Haki za Binadamu, Masuala ya Katiba na Sheria Edson Macuacua amewaambia wabunge kuwa, kwa kupitishwa sheria hiyo, idadi ya wasichana wanaoacha shule na kulazimishwa kuolewa wakiwa na umri mdogo itapungua. Amesema hii itasaidia kujenga jamii yenye haki ambako wavulana na wasichana wana fursa sawa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |