Umoja wa Mataifa umelaani shambulizi la kigaidi lililotokea Ijumaa iliyopita mjini Mogadishu, Somalia, na kusababisha vifo vya watu 26, na wengine 56 kujeruhiwa.
Mjumbe maalumu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni kiongozi wa tume ya msaada ya Umoja huo nchini Somalia Bw. James Swan amesema, mashambulizi ya kigaidi hayawezi kuvuruga juhudi za kuleta utulivu nchini Somalia.
Naye mkurugenzi mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji IOM Bw. Antonio Vitorino pia amelaani vikali shambulizi hilo, ambalo limewaua watu wengi akiwemo mfanyakazi mmoja wa shirika hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |