Kamati ya afya ya mkoa wa Guangdong imetangaza kuwa serikali ya Guinea ya Ikweta imewapatia wafanyakazi wote 29 wa kikundi cha madaktari wa China, tuzo ya juu kabisa nishani ya Uhuru ya Taifa ili kusifu mchango uliotolewa na kikundi hicho kwa sekta ya afya ya nchi hiyo.
Katika mwaka mmoja na nusu uliopita, madaktari wa kikundi hicho wamewatibu wagonjwa 7,689, kufanya upasuaji 1,349, kuwaokoa wagonjwa mahututi 116, na kutoa tiba ya akyupancha kwa watu 1420. Aidha timu hiyo imetoa mafunzo maalum kuhusu matibabu ya dawa za Kichina, ili kueneza matibabu ya jadi ya Kichina, na kuwanufaisha zaidi watu wa Guinea ya Ikweta kutokana na huduma za matibabu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |