• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kigali kuwa mwenyeji wa jukwaa la Biashara la Kimataifa mwezi ujao

    (GMT+08:00) 2019-07-16 20:17:00
    Wawekezaji wa ngazi za juu na watunga sera kutoka sehemu mbalimbali duniani mwezi ujao watakusanyika jijini Kigali kwa ajili ya Jukwaa la Biashara Duniani litakalofanyika tarehe 9 Agosti katika jumba la Mikutano la Kigali Convention Centre,ili kujadiliana kuhusu jinsi sekta binafsi inavyoweza kuongeza mchango wake katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi barani Afrika.

    Jukwaa hili la biashara linaandaliwa na Shirikisho la Sekta Binafsi Rwanda chini ya kaulimbiu ya "Kufungua Biashara ya Afrika,Yenyewe ,na Ulimwengu" kama kongamano la kila mwaka ambalo linawaleta pamoja wadau mbalimbali kujadiliana,kugundua fursa,na kubadilishana uzoefu wa namna uchumi unaosukumwa na sekta binafsi unaweza kuwa na ufanisi.

    Mkutano huo utaleta pamoja washiriki takriban 1000 kutoka Afrika,Asia,Ulaya,na Amerika.

    Mada zitakazojadiliwa ni pamoja na faida ya ushindani wa bara la Afrika-soko moja kubwa na mkataba wa biashara huru,na hali ya uzoefu wa kibiashara wa Afrika na China na jinsi China ilivyojiimarisha kufanya biashara na Afrika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako