• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kanda ya Maziwa Makuu barani Afrika yaahidi uwazi katika mchakato wa uchaguzi

    (GMT+08:00) 2019-07-17 09:22:43

    Nchi zilizo kwenye kanda ya Maziwa Makuu zimeahidi kuongeza uwazi katika mchakato wa uchaguzi ili kuimarisha amani, utulivu, ujumuishi na maendeleo endelevu.

    Wabunge na wataalam kutoka kanda hiyo wamesema katika mkutano wao uliofanyika Nairobi, Kenya, kuwa kuboresha usimamizi wa uchaguzi ni ufunguo wa kuzuia vurugu ambazo zinatishia mshikamano na maendeleo.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Bi. Monica Juma amesema, chaguzi zinazofanyika kwa uhuru, usawa na uwazi ni hitaji muhimu la kudumisha utulivu, amani na maafikiano katika kanda ya Maziwa Makuu.

    Amesema kuboresha mchakato wa uchaguzi katika kanda hiyo kupitia matumizi ya teknolojia na ushirikishwaji mkubwa wa wananchi kutaongeza kasi ya ushirikiano kati ya nchi zinazokabiliwa na migogoro ya kisiasa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako