Bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Fedha la Kimataifa IMF imesema hivi karibuni itaanza mchakato wa kumchagua mkurugenzi mtendaji mpya baada ya mkurugenzi wa sasa Bi. Christine Lagarde kuwasilisha barua ya kujiuzulu wadhifa wake katika Shirika hilo muda wake utakapokamilika Septemba, 12 mwaka huu. Wiki mbili zilizopita, Lagarde alipendekezwa kuwa rais wa Benki Kuu ya Ulaya, ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya viongozi wa Umoja wa Ulaya juu ya uongozi wa baadaye wa taasisi za ngazi ya juu za Umoja huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |